KOCHA wa Chelsea, Guus Hiddink ameeleza            kwamba kocha mwenzake wa Leicester City, Claudio Ranieri            alimpigia simu kumshukuru mara baada ya mechi yao dhidi ya            Tottenham kumalizika kwa sare ya 2-2 Jumatatu usiku.
        Matokeo hayo yaliyokuja baada ya Chelsea            kuwa nyuma kwa mabao 2-0 hadi mapumziko, yameiwezesha            Leicester kuwa mabingwa wa Premier League kwa mara ya kwanza,            na kuwa habari kubwa katika soka ya England.
         "Mara            tu baada ya mechi, baada ya filimbi ya mwisho, nilipata simu            kutoka kwa Ranieri," alisema Hiddink na kuongeza kuwa kocha            huyo wa Leicester alikuwa na furaha sana kwa juhudi            walizoonyesha dhidi ya Spurs.
        "Alitushukuru kwa tulichofanya, hasa            katika kipindi cha pili. Nilimpongeza kwa kuwa bingwa… Alikuwa            na hisia. Sikuona machozi kwa sababu hayakuwa mazungumzo ya            ana kwa ana, lakini sauti yake ilikuwa na tetemeko kidogo,            ndiyo.
        "Alisema shukrani mara tano kwa sababu            hisi zilikuwa zinazidi kupanda."
        
Comments
Post a Comment