Utawala wa Pep Guardiola katika klabu ya Bayern Munich angalau kwa upande wa michuano ya Champions League umefikia mwisho. Kocha huyo mkatalunya, ambaye alimrithi mshindi wa makombe matatu ya kihistoria Jupp Heynckes, ameshindwa kufikia mafanikio ya mtangulizi wake na sasa ataondoka kwenda kujiunga na Manchester City bila kutimiza ndoto yake na ya mashabiki wa Bayern ya kushinda ubingwa mwingine wa ulaya miaka 3 baada ya kujiunga na Bavarians.
  Rekodi nzuri ya makombe ilikuwa ndio ngao kuu ya          kumlinda kocha huyu mwenye umri aa miaka 45 na falsafa zake za          soka, ambazo zilikuwa zikiwapa mashaka na baadhi ya wadau kama          vile wachezaji, mashabiki, legends kama vile Franz Beckenbauer          na Karl Heinz Rummenigge.
"Tutakuja kuwa hatuangaliziki kama Barca. Hakuna atakayetaka kutuangalia, kwa sababu wachezaji watakuwa wanacheza kwa kupiga pasi za kurudi nyuma," Kaiser alisema baada ya Pep kuteuliwa kushika madaraka, kabla hajaja kubadilisha maneno na kusifu mbinu za kocha huyo wa kihispaniola.
Pamoja na kushinda Bundesliga kila msimu katika miaka yake yote pale Allianz Arena, pia kombe la ligi mwaka 2014, utawala wa Guardiola umekuwa na bahati mbaya ya kutolewa mara tatu mfululizo katika Champions League hatua ya nusu fainali na vilabu vya Hispania.
  Real Madrid walikuwa wa kwanza kuwa kizingiti          cha Pep Guardiola kuingia fainali mwaka 2014 kwa kuwapa Bayern          kipigo cha 0-4 @Allianz Arena. Kikosi cha Luis Enrique cha          Barcelona wakafuatia kuiondoa Bayern nje ya mashindano kwa          kuwafunga 3-0 Camp Nou na 3-2 Allianz Arena katika hatua ya nusu          fainali.
  Hatimaye jana usiku Atletico Madrid nao          wamefanikiwa kuiondoa Bayern katika nusu fainali ya michuano ya          Champions League msimu huu kwa kuwafunga 1-0 Vicente Carlderon          na usikua wa kuamkia leo wakafungwa 2-1 lakini wakafuzu kwa goli          la ugenini. 
 
          Katika miaka yote hii timu ambayo iliifunga Bayern huenda na          kutwaa ubingwa wa ulaya, Je Atletico ataweza kuzitafuna aidha          Real Madrid au Manchester City.
Comments
Post a Comment