STAA mpya wa              Arsenal, Granit Xhaka amesema ligi ya Uingereza itamfaa              kwasababu ni mchezaji mwenye nguvu na anayependa kupambana.
        Arsenal Jumatano              hii walitangaza kwamba wamefanikiwa kiumsajili mchezaji huyo              raia wa Uswisi kutoka Borusia Monchengladbach, anayetua              akitokea Bundesliga na sifa kama mchezaji mahiri katika              kukaba dimbani.
        "Napenda uchezaji              wa Ligi ya Uingereza, ni soka la kibabe," alisema Xhaka              kaytika mahojiano yake ya kwanza kwenye tovuti ya klabu.
        "Ni mapambano,              napenda sana lakini pia Arsenal ni klabu inayocheza mpira wa              hali ya juu na hiyo ni nzuri sana."
        "Katika Ujerumani              utacheza soka la kibabe lakini mara nyingi mwamuzi hupuliza              kipyenga lakini kwa Uingereza haiku hivyo, hii ni njema sana              kwangu."
        Xhaka anatarajia              kuimarisha kikosi cha Arsenal ambacho kimetajwa kuwa nyororo              sana, mara nyingi amefanya makabiliano 'tackle' 244 katika              mechi 108 alizocheza Bundesliga.
        Hata hivyo aina              yake ya uchezaji imemuingiza matatizoni mara kadhaa kwani              ametolewa mara tano kwa kadi nyekundu Bundesliga.
        Xhaka aliiongoza              Gradbach kumaliza nafasi ya nne msimu uliopita na amesema              yuko tayari kupewa kitambaa cha unahodha Arsenal pia.
        
Comments
Post a Comment