MLINZI wa katikati wa klabu ya Villareal ya Hispania,            Eric Bailly amewaambia Real Madrid kuachana na azma yakutaka            kumng'oa kwasababu bado hana sababu ya kutaka kuachana na timu            yake ya sasa.
        Kwa msisitizo Eric Bailly amesema kuwa anajisikia            furaha na maisha ndani ya Villareal.
        "Taarifa hizo za klabu nyingi kunihitaji zinanipa            faraja na heshima kubwa, lakini dhamira yangu ya sasa ni            kuendelea kubaki hapa kwani bado nina kandarasi ya mwaka unusu            kuendelea kuwepo Villareal," alisisitiza.
        Kwa sasa beki huyo mwenye umri wa miaka 21 anatajwa            katika dili la usajili Real Madrid.
        Madrid wametajwa katika mpango wa kuimarisha kikosi            chao na Zinedine Zidane amesema Bailly ni kati ya walinzi            imara wa kuwajumlisha katika kikosi cha msimu ujao.
        Raia huyo wa Ivory Coast alithibitisha kusikia taarifa            za kutakiwa na wakongwe hao lakini alikanusha kuhusu kukubali            kujiunga nao katika majira ya kiangazi.
        "Sifahamu lolote juu ya tetesi hizo japo nimezisikia,"            Bailly aliliambia AS.
        "Ninachojua ni kwamba ninataka kumaliza kandarasi yangu            nikiwa na Villareal. Hii ni klabu yangu, bado nina mkataba wa            miaka miwili, nina furaha kuwa hapa."
        
Comments
Post a Comment