Kipa wa MANCHESTER UNITED  David de Gea                huenda akaandoka Old Trafford kiangazi hiki iwapo Louis                van Gaal ataendelea kuwa kocha wa klabu hiyo msimu ujao.
            Van Gaal bado ana mwaka mmoja kwenye                mkataba wake na kuna matarajio madogo kuwa atapewa nafasi                ya kumaliza mkataba huo.
            Ingawa Van Gaal anaamini kuwa De Gea                yuko na furaha Old Trafford, lakini watu wa karibu na                mlinda mlango huyo wanabainisha kuwa kuendelea kuwepo kwa                Van Gaal kutafungua milango wa De Gea kutimka Manchester                United.
            Inaelezwa kuwa De Gea, kipa wa                kimataifa wa Hispania mwenye umri wa miaka 25, haamini                katika mfumo wa Van Gaal.
            
Comments
Post a Comment