Cristiano                Ronaldo amemkingia kifua kocha mpya ajaye Manchester              United Jose Mourunho kwa kusema huyo ndiye mtu sahihi wa              kuirejesha klabu hiyo katika enzi za kuzoa mataji.
        Mourinho anakuwa            kocha mpya wa United kufuatia kutimuliwa kwa Louis van Gaal na            licha ya jina la Mourinho kupokelewa kwa hisia tofauti na            wachambuzi wa soka, Ronaldo amewatoa shaka mashabiki wa timu            yake hiyo ya zamani kwa kusema Mreno mwenzake ndiye mtu sahihi            kwa sasa Old Trafford.
        Ronaldo            aliyetumikia United kwa miaka sita ya mafanikio makubwa,            amesema Mourinho ni chaguo bora zaidi.
        Manchester United              inajiandaa kumtangaza Jose Mourinho kama kocha wake mpya
        Cristiano Ronaldo              anatumai kuwa Mourinho ataleta mataji United. 
        
Comments
Post a Comment