Manchester United            imepigwa kumbo la mwaka baada ya Bayern Munich kumsajili            kiungo wa Benfica Renato Sanches ambaye iliaminika anakwenda Old Trafford.
        Renato Sanches            mwenye umri wa miaka 18, amesaini mkataba wa miaka mitano            kuitumikia Bayern Munich katika dili litakalopanda hadi            kufikia thamani ya pauni milioni 63.
        Hadi mwanzoni mwa            wiki hii, Sanchez alikuwa akitwajwa kukamilisha safari ya            kujiunga na Manchester United ambayo imekuwa ikimfuatilia            kinda huyo kwa msimu mzima, lakini kwa maajabu ya wengi,            Bayern Munich ikaibuka ghalfa na kumnyakua kiungo huyo mwenye            kipaji cha aina yake.
        Bayern Munich              imetangaza kumsajili Renato Sanches kutoka Benfica kwa pauni              milioni 28 - Nyota huyo wa kimataifa wa Ureno amesaini              mkataba huo mbele ya mtendaji mkuu wa Beyern Karl-Heinz              Rummenigge
        Sanches akipozi na              Rummenigge baada ya kusaini mkataba wa miaka mitano
        Sanches akifanya vipimo              vya afya Bayern Munich 
          
Comments
Post a Comment