MAISHA ni popote,              ukona upande mmoja umebana, unageukia upande mwingine              ilimradi maisha yasonge mbele.
        Ndivyo unavyoweza              kusema baada ya nyota mmoja katika kikosi cha Manchester              United ambaye anaandamwa na majeruhi, sasa ameamua kuanza              maisha mapya wakati akiendelea kujiuguza.
        Habari zinasema              kwamba nyota huyo Bastian Schweinsteiger anajiandaa kucheza              tangazo jipya la iPhone app, Clash of Kings.
        Mchezaji huyo wa              kimataifa wa Ujerumani akiwa na kikosi cha Old Trafford              ndani ya msimu wake wa kwanza kwenye premier league              hajafurahia maisha yake mapya kwenye Ligi hiyo kutokana na              kuandamwa na majeruhi ya mara kwamara huku kukiwa na taarifa              huenda akaikosa michuano ya euro 2016 itakayoanza mwezi Juni              nchini Ufaransa.
        Kiungo huyo              mwenye miaka 31, anatarajiwa kukaa nje ya uwanja kwamuda              mrefu zaidi katika maisha yake ya soka na muda huo atautumia              kutengeneza tangazo jipya la Clash of Kings.
        Kwa mujibu wa              gazeti la Bild la nchini Ujerumani, Schweinsteiger atacheza              kama mfalme kwenye tangazo hilo la kibiashara huku akiwataka              watu waunganishe program hiyo ya gemu na kucheza.  
        Bado haijawekwa              wazi kwamba ni lini tangazo hilo litaachiwa, lakini litakuwa              linavutia kumuona Schweinsteiger kwenye sehemu ya tangazo              hilo.
        Mchezaji huyo ni              kama anafuata nyayo za mchezaji wa zamani wa Manchester              United, Eric Cantona kuamua kucheza muvi baada ya kutundika              daruga.
        
Comments
Post a Comment