ATLETICO Madrid              itakuwa miongoni mwa klabu zitakazofaidika kwa ukubwa zaidi              kwenye dili jipya la uuzaji wa haki za matangazo ya              televisheni ya mechi za Ligi Kuu ya Hispania La Liga.
        Kwa mujibu wa              ripoti inaaminika kwamba Atletico walikuwa wakipata kiasi              cha euro milioni 45 mpaka kufikia kiasi cha milioni 100 kwa              mwaka.
        Los Lojiblancos,              mabingwa wa La Liga miaka miwili iliyopita bado wapo kwenye              nafasi nzuri ya kutwaa ubingwa wa mara nyingine msimu huu na              wamefaidika zaidi kutokana na sheria mpya za mgawanyo wa              fedha ambao umetengenezwa ili kuweka usawa kwa kiasi fulani              mongoni mwa klabu.
        Fedha hizi              zitakuza pato mpaka kuzidi mapato ya timu kama mabingwa wa              Ujerumani, Bayern Munich ambao wanapokea kiasi cha euro              milioni 50 na mabingwa wa Italia, Juventus ambao wnapokea              kiasi cha euro milioni 94.
        Ni klabu kubwa tu              za premier league, mashindano tajiri zaidi duniani, ambao              watapokea fedha nyingi zaidi ya Atletico zikiwemo Manchester              United, Manchester City na Chelsea ambao watapokea kiasi cha              zaidi ya euro milioni 165.
        Kanuni mpya              ambazo zitaanza kutumika kuanzia msimu ujao zitapunguza              nguvu za Madrid na Barcelona ambao wao hupokea kiasi cha              euro milioni 140 kila timu na timu nyingine kidogo kama              Eibar watakuwa wakipokea kiasi cha euro milioni 43 badala ya              euro milioni 18 wakati Sevilla watapokea kiasi cha euro              milioni 60.
        
Comments
Post a Comment