INGAWA inawezekana kuwa            ni ndoto za alinacha, lakini bado bosi wa Washika Mitutu wa            jiji la London, Arsene Wenger anaamini kukamilika kwa ndoto            aliyoanza miaka mingi nyuma ya kumnasa Lionel Messi.
        Ndoto za Mfaransa              huyo zimekuja siku chache baada ya kubainisha azma ya              kumwita kundini nyota huyo raia wa argentina. Katika mpango              wake wa miaka mitano nyuma, Wenger alikuwa akimfukuzia nyota              huyo wa Barcelona ingawa mpango wake huo ulizimwa bila ya              mafanikio.
        Lakini hata sasa              Wenger amekiri kuvutiwa na mpachika mabao huyo mwenye              heshima na hadhi kubwa kwa sasa ulimwenguni kote.
        Katika kunukuliwa              kwake, bosi huyo alisema alijaribu kumsajili Lionel Messi              kama mpango wa kutaka kuwanyakua wachezaji watatu wachanga              wa klabu hiyo.
        Messi alikuwa na              miaka 15 wakati huo na mwenzake Gerrad Pique pamoja na              aliyekuwa kiungo wa kati wa Arsenal, Cess Fabregas.
        Wenger: "Tulitaka              kumchukua Fabregas, Messi na Pique lakini tukafanikiwa              kumpata Fabregas pekee."
        Wenger aliongeza:              "Nadhani Messi mwenyewe hakutaka kujiunga nasi."
        Fabregas              alichezea klabu ya Arsenal kwa miaka minane kabla ya kurudi              Barcelona, huku Pique akijiunga na Manchester United mwaka              2004.
        Messi mwenye umri              wa miaka 27, amechezea timu ya Barcelona kwa muda wote na              kuisaidia kushinda mataji sita ya La Liga pamoja na Kombe la              Klabu Bingwa mara tatu baada ya mpango wa kujiunga na              Arsenal kugonga mwamba.
        Hata hivyo Wenger              amepinga madai kwamba mpango huo ulifeli kutokana na              matatizo ya Messi na familia yake.
        "Messi ni              mchezaji mkubwa nakubali kuhusu ukweli huu, lakini Arsenal              nayo ni klabu kubwa ambayo ina uwezo wa kumsajili mchezaji              huyu."
        "Nimekuwa na              ndoto hii tangu zamani na hata sasa, ninaamini kuwa uwezo na              sababu hii bado ninayo na hata mipango ya awali niliyoanza              ninaweza kuiendeleza katika muda muafaka."
        "Muda unaweza              kufikia ni jambo la kusubiri na kuvuta subira. Isiwe msimu              ujao lakini mwisho wa siku kuna jambo linaweza kutokea              kuhusiana na hatua yangu hii ya kuwa na nyota mkubwa, bila              shaka anaweza kuwa Lionel Messi," amenukuliwa Wenger.
        Huenda taarifa              hizi zinakuja katika siku hizi ambazo kikosi cha Arsenal              kimejizatiti katika kuhakikisha kinakuwa na matokeo mazuri              ifikapo mwisho wa msimu huu ingawa wamepoteza mchezo wa              mwishoni mwa juma lililopita.
        
Comments
Post a Comment