YAYA TOURE AWAFUNIKA WENZAKE MANCHESTER CITY KWA MAGARI YA KIFAHARI



YAYA TOURE AWAFUNIKA WENZAKE MANCHESTER CITY KWA MAGARI YA KIFAHARI
 Manchester City            midfielder Yaya Toure's standing at the club risks being            undermined by his agent

YAYA TOURE ni 'mlevi' wa magari ya kifahari na sasa amewafunika mastaa wenzake wa Manchester City katika eneo la maegesho ya magari la klabu hiyo akiwa na Rolls Royce mbili zenye thamani ya jumla ya pauni 600,000.

Kiungo huyo raia wa Ivory Coast mwenye miaka 32, tayari alikuwa na Rolls Royce Wraith yenye thamani ya pauni 250,000 lakini akafunikwa na Samir Nasri aliyenunua Lamborghini Aventador kwa pauni 330,000.

Sasa Toure amefungua tena pochi yake na kununua Rolls Royce Phantom kwa pauni 350,000 na kumfanya kumiliki magari ya kifahari yenye thamani ya jumla ya pauni milioni 1.

Miezi 12 iliyopita, Toure ambaye anahusishwa kuondoka Etihad kiangazi hiki, alionekana akiendesha Mercedes G Class jeep yenye thamani ya pauni 150,000, Mercedes Brabus 850 ya pauni 300,000, Bentley Continental ya pauni 200,000 na Porsche Carerra ya pauni 90,000.

Staa huyo anayelipwa mshahara wa pauni 220,000 kwa wiki, Jumatatu wiki hii ameonekana akiendesha Rolls Royce Phantom nyeusi akielekea mazoezini.


Comments