LOUIS VAN GAAL amefurahi "kuona furaha"            katika macho ya wachezaji wake na mashabiki wa Manchester            United baada ya kupata ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Everton            katika nusu fainali ya FA Cup iliyopigwa Wembley Jumamosi            jioni.
        Akizungumza na BBC Sport baada ya filimbi            ya mwisho, Van Gaal alisema: "Wakati unapoona furaha katika            macho ya wachezaji, ni nzuri sana, lakini pia kwa mashabiki.            Nadhani tulistahili kwenda katika fainali."
        Hata hivyo kocha huyo alisema kuwa            hakufurahishwa na refa kwa jinsi alivyochezesha mechi hiyo            kwamba alibadili mchezo kwa "kuwanyima faulo".
        Anthony Martial alifunga mwishoni kumaliza            mchezo baada ya awali kumtengenezea nafasi Marouane Fellaini            kuipa United uongozi wa 1-0. 
        Everton walipoteza penalti wakati ubao            ukionyesha wako nyuma kwa 1-0, baada ya David De Gea kuokoa            shuti la Romelu Lukaku, lakini wakafanikiwa kusawazisha kwa            Chris Smalling kujifunga kabla Martial kuwaliza.
        
Comments
Post a Comment