Taji              la FA linaweza likampa faraja kocha wa Machester United              Louis van Gaal, lakini inaaminika halitamwokoa katika              kupigania kibarua chake Oldt Trafford.
        United              inajitupa kwenye dimba la Wembley hapo baadae kuchuana na              Everton katika nusu fainali ya FA Cup  na ingawa kikosi cha              Van Gaal kinapewa nafasi kubwa ya ushindi, lakini ni nafasi              ya nne kwenye Top Four ya Premier League ndiyo inayoweza              kumwokoa kocha huyo wa Uholanzi.
        Wachambuzi wa soka            England wanaendelea kumuhusisha kwa kiasi kikubwa kocha Jose            Mourinho na kibarua cha kuikochi United msimu ujao.
        Van Gaal amekuwa            akijipa moyo kutokana kuimarika kwa ubora wa kikosi chake,            lakini bado ana kazi kuwa ya kuishawishi bodi ya Manchester            United isimuonyeshe mlango wa kutokea.
        Kocha huyo            amebakiza mwaka mmoja katika mkataba wake wa miaka mitatu Old            Trafford.
        Nahodha Wayne Rooney              akipokea maelekezo ya kocha wa Manchester United kabla ya              kuelekea kwenye mchezo wa FA dhidi ya Everton
        
Comments
Post a Comment