TOTTENHAM YAITENGEA UBINGWA LEICESTER CITY …yalazimishwa sare na West Brom …Man United na Chelsea ‘kumtangaza’ bingwa Jumapili na Jumatatu ijayo


TOTTENHAM YAITENGEA UBINGWA LEICESTER CITY …yalazimishwa sare na West Brom …Man United na Chelsea 'kumtangaza' bingwa Jumapili na Jumatatu ijayo

West            Brom celebrate after drawing level after Hugo Lloris was            caught out coming for a corner, and Dawson headed home

TOTTENHAM imeitengea ubingwa Leicester City. Ndivyo unavyoweza kusema baada klabu hiyo kushindwa kuutumia vema uwanja wake wa nyumbani White Hart Lane na kulazimishwa sare ya 1-1 na West Bromwich katika mchezo wa Ligi Kuu ya England.

Mchezaji Craig Dawson wa West Bromwich ndiye aliyefunga magoli yote mawili ambapo alianza kwa kujifunga dakika ya 33 kabla hajawa shujaa kwa kuisawazishia timu yake dakika ya 73.

Leicester sasa inaweza ikatwaa ubingwa Jumapili iwapo itafunga Manchester United, lakini hata ikipoteza mechi hiyo bado itahitaji pointi tatu tu katika michezo yake itakayofuta ili kufikisha pointi 79 ambazo ambazo hazitafikiwa na Tottenham yenye pointi 69.

Timu zingine zote zilizosalia zimeshapoteza nafasi ya kutwaa ubingwa, jambo ambalo pia liko njiani kutokea kwa Tottenham.

Tottenham ilihitaji ushindi katika mchezo dhidi ya West Bromwich ili kuendelea kuipumulia Leicester City.

Leicester City pia itakuwa na nafasi ya kutwaa ubingwa hata kama itafungwa na United Jumapili halafu Tottenhm ikafungwa na Chelsea Jumatatu ijayo.
Boaz Myhill cannot prevent                  the balls slipping through his legs after Craig Dawson                  had forced it towards his own goal to put Spurs ahead
Boaz Myhill cannot prevent the balls slipping through his legs after Craig Dawson had forced it towards his own goal to put Spurs ahead
Jan Vertonghen wa Tottenham (katikati)anashangilia baada kumpa presha Dawson hadi akajifunga
Dawson anaruka juu ya mabeki wa Tottenham na kufunga tena lakini safari hii ni bao la kusawazisha kwa timu yake West Brom 
Msimamo wa ligi ulivyo 




Comments