SIR ALEX FERGUSON ALICHEMKA KUMWACHIA PAUL POBGA ...aliiondoka bure lakini leo thamani yake ni pauni mil 100
Paul Pogba            anawindwa na Barcelona katika kipindi hiki ambacho inaonekana            yupo tayari kuondoka Juventus kiangazi hiki. 
        Kwa sasa Pobga            kinda wa zamani wa Manchester United anatajwa kuwa na thamani            ya pauni milioni 100, hatua inayowafanya wachambuzi wa soka            waamini kuwa kocha wa zamani wa United Sir Alex Ferguson            alifanya kosa kubwa kumwacha nyota huyo aondoke bure.
        Akiwa Manchester            United, Pobga hakupewa nafasi na            Ferguson ya kuanza katika mchezo wowote ule wa timu ya wakubwa            zaidi ya kucheza mechi chache sana akitokea benchi.
        Kiungo huyo            akaamua kutimka na kujinga na Juventus mwaka 2012 na kuibuka            kuwa shujaa aliyeweza kucheza mechi 121 na kufunga magoli 28.
        United ni moja ya            timu za Ulaya zinazotajwa kuwania saini ya Pobga lakini            mashabiki wake wengi wamekuwa wakiumizwa na matamanio ya klabu            yao kutaka kumwaga pesa ndefu kwa mchezaji waliyempuuza na            kumwacha aondoke bure.
        Enzi hizo: Paul Pogba              (wa pili kushoto), aliondoka Manchester United bila kuanza              katika mechi yoyote ya wakubwa lakini sasa ni mchezaji lulu              duniani anayetamaniwa na vilabu vyote vikubwa barani Ulaya.              Picha hii ni ya mwaka 2011 baada ya kushinda kombe la FA la              Vijana FA. Wengine pichani Ryan Tunnicliffe (kushoto), Jesse              Lingard wa pili kushoto na Ravel Morrison
        Inadaiwa Ferguson              alikataa wazo la wakala wa Pobga aliyetaka mchezaji wake              alipwe pauni 20,000. Pichani ni Pogba akicheza mechi ya              Premier League dhidi ya West Brom  2012
          
Comments
Post a Comment