SIR ALEX FERGUSON ALICHEMKA KUMWACHIA PAUL POBGA ...aliiondoka bure lakini leo thamani yake ni pauni mil 100



SIR ALEX FERGUSON ALICHEMKA KUMWACHIA PAUL POBGA ...aliiondoka bure lakini leo thamani yake ni pauni mil 100

Paul Pogba anawindwa na Barcelona katika kipindi hiki ambacho inaonekana yupo tayari kuondoka Juventus kiangazi hiki. 

Kwa sasa Pobga kinda wa zamani wa Manchester United anatajwa kuwa na thamani ya pauni milioni 100, hatua inayowafanya wachambuzi wa soka waamini kuwa kocha wa zamani wa United Sir Alex Ferguson alifanya kosa kubwa kumwacha nyota huyo aondoke bure.

Akiwa Manchester United, Pobga hakupewa nafasi na Ferguson ya kuanza katika mchezo wowote ule wa timu ya wakubwa zaidi ya kucheza mechi chache sana akitokea benchi.

Kiungo huyo akaamua kutimka na kujinga na Juventus mwaka 2012 na kuibuka kuwa shujaa aliyeweza kucheza mechi 121 na kufunga magoli 28.

United ni moja ya timu za Ulaya zinazotajwa kuwania saini ya Pobga lakini mashabiki wake wengi wamekuwa wakiumizwa na matamanio ya klabu yao kutaka kumwaga pesa ndefu kwa mchezaji waliyempuuza na kumwacha aondoke bure.

The one that got away: Paul                  Pogba, second right, left Manchester United without                  starting a senior game and is now one of the world's                  most coveted players. He is pictured in 2011 after                  winning the FA Youth Cup with Ryan Tunnicliffe, left,                  Jesse Lingard, second left, and Ravel Morrison
Enzi hizo: Paul Pogba (wa pili kushoto), aliondoka Manchester United bila kuanza katika mechi yoyote ya wakubwa lakini sasa ni mchezaji lulu duniani anayetamaniwa na vilabu vyote vikubwa barani Ulaya. Picha hii ni ya mwaka 2011 baada ya kushinda kombe la FA la Vijana FA. Wengine pichani Ryan Tunnicliffe (kushoto), Jesse Lingard wa pili kushoto na Ravel Morrison
Ferguson reportedly                    refused to bow to agent Mino Raiola's wage demands of                    around £20,000 a week. Pogba failed to start a single                    game but is pictured in Premier League action against                    West Brom in 2012
Inadaiwa Ferguson alikataa wazo la wakala wa Pobga aliyetaka mchezaji wake alipwe pauni 20,000. Pichani ni Pogba akicheza mechi ya Premier League dhidi ya West Brom  2012




Comments