REAL MADRID YASAKA REKODI MPYA LA LIGA


REAL MADRID YASAKA REKODI MPYA LA LIGA
Real            Madrid's Cristiano Ronaldo, right, vies for the ball with            Villarreal's Daniele Bonera during a Spanish La Liga soccer            match between Real Madrid and Vill...
REAL MADRID inatafuta kuandika rekodi ya kihistoria katika La Liga, ya kushinda mfululizo mechi 12 za mwisho, mafanikio ambayo hayajafikiwa na timu nyingine yoyote.
Tayari Madrid imeshinda mechi nane mfululizo dhidi ya Levante, Celta, Las Palmas, Sevilla, Barcelona, Eibar, Getafe na Villarreal, ikibakiwa na mechi nne dhidi ya Rayo Vallecano, Real Sociedad, Valencia na Deportivo La Coruna.
Timu ya kwanza kuandika rekodi ya kushinda mechi nyingi mfululizo mwishoni mwa msimu wa ligi ni Barcelona iliyofanya hivyo msimu wa 1959/60 ambapo ilishinda mechi zake nane za mwisho.
Barcelona ambayo kabla ya kushinda mechi hizo ilikuwa nafasi ya pili katika msimamo wa ligi, ilimaliza ikiwa bingwa.
Villarreal iliifikia rekodi hiyo ya Barcelona msimu wa 2006/07, ambapo ikiwa katikati ya msimamo ilishinda mfululizo mechi nane za mwisho na kupanda hadi katika nafasi ya kushiriki michuano ya Ulaya.
Real Madrid ikiwa katika ubora wake, ilifanikiwa kushinda mfululizo mechi saba za mwisho na kumaliza ikiwa bingwa wa ligi mara mbili katika misimu ya 1980/81 na 2011/12.


Comments