RAIS wa zamani wa Real Madrid, Lorenzo            Sanz, amekoleza 'vita' kati ya timu yake na Atletico Madrid            msimu huu, kwa kueleza kuwa anawataka wapinzani wao hao wa mji            mmoja katika fainali ya Champions League kwa kuwa ni rahisi            kuwafunga.
        Klabu hizo mbili kwa sasa zinapigana vita            inayofanana, kila moja ikijaribu kutwaa taji la La Liga kutoka            kwa Barcelona na pia kufika fainali ya Champions League.
        Sanz, ambaye alikuwa rais wa Real kutoka            1985 hadi 1995 na kuwa mwenyekiti kutoka 1995 hadi 2000,            alifanikiwa kupata mafanikio wakati timu hiyo iliposhinda            Champions League mwaka 1998 na 2000.
        Na sasa Mhispania huyo anaamini kwamba            fainali inayowezekana kati ya Real na Atletico itamalizika kwa            matokeo ya aina moja tu – ushindi kwa Real.
        "Natarajia Atletico itafika fainali ya            Champions League kwa sababu tunaweza kuwafunga… Tutashinda            taji la 11 (Champions League)," alisema Sanz akijiamini.
        
Comments
Post a Comment