REAL MADRID IKO TAYARI KUMUUZA JAMES RODRIGUEZ MANCHESTER UNITED


REAL MADRID IKO TAYARI KUMUUZA JAMES RODRIGUEZ MANCHESTER UNITED
James Rodriguez            celebrates giving Real Madrid the lead in the 4-0 victory over            Eibar at the Santiago Bernabeu
MWANDISHI na mchambuzi maarufu wa soka raia wa Hispania, mwenye rekodi ya kuibua stori za usajili, Guillem Balague, amesema Real Madrid iko tayari kumuuza staa wake James Rodriguez kwa Manchester United kiangazi hiki, kama wataweka mezani dau nono.

Kiungo huyo mchezeshaji wa zamani wa Monaco, amekuwa na msimu wa misukosuko Bernabeu na wiki iliyopita alionywa na kocha wake, Zinedine Zidane baada ya kucheka akiwa kwenye benchi wakati Madrid ikichapwa 2-0 na Wolfsburg katika mechi ya kwanza ya robo fainali ya Champions League.

Staa huyo raia wa Colombia mwenye miaka 24, alichagua kuhamia kwa miamba hiyo ya La Liga akiungana na Gareth Bale na Cristiano Ronaldo kuunda safu ya ushambuliaji badala ya kutua Premier League baada ya kung'ara katika World Cup in 2014.

Kutokana na uwezo wake ina maana kwamba licha ya kuwa na msimu mbaya, Red Devils bado wana hamu ya kumpata staa huyo wa zamani wa Porto, na Balague ambaye aliibua stori kubwa za usajili kama kutua kwa Angel Di Maria Old Trafford, amesema Madrid haina tatizo na kumuuza kiangazi hiki kama Manchester United itafika bei.


"Ninachoweza kusema ni kwamba Real Madrid ina zaidi ya furaha kumuuza Rodriguez… kama watapata kiasi sahihi cha fedha," Balague aliiambia televisheni ya Sky Sports.


Comments