WAYNE Rooney amemkuna            Louis van Gaal aliposhika dimba la kati katika mechi ambayo            Manchester United wameshinda 2-0 dhidi ya Crystal Palace            Jumatano usiku, na sasa nafasi hiyo inamuhusu straika huyo.
        Kutokana na            kumthibitisha Marcus Rashford kuwa chaguo la kwanza katika            nafasi ya mshambuliaji wa kati, Van Gaal amekiri kuwa            amelazimika kumtafutia Rooney majukumu mengine katika nusu            fainali ya FA Cup dhidi ya timu yake ya zamani ya Everton            Jumamosi.
        "Hakuna mchezaji mwenye            nafasi ya kudumu, natumia wachezaji ambapo nadhani wanaweza            kutoa mchango mkubwa zaidi katika mechi fulani. (Rooney)            alikuwa na jukumu kwenye kiungo kutokana na namna Crystal            Palace walivyocheza.
        "Sitaki kumbadili            (Marcus) Rashford kama straika. Inabidi kuangalia nafasi            nyingine kwa Wayne. Alifanya hivyo mwaka uliopita (kucheza            kiungo), hivyo si jambo jipya kwangu. Nina furaha sana kwa            jinsi alivyocheza," alisema Van Gaal.
        
Comments
Post a Comment