PICHA 18 ZA TASWIRA YA MSIBA WA NDANDA KOSOVO JUMANNE USIKU ...ratiba ya mazishi yawekwa hadharani


PICHA 18 ZA TASWIRA YA MSIBA WA NDANDA KOSOVO JUMANNE USIKU ...ratiba ya mazishi yawekwa hadharani

Msiba wa mwanamuziki Ndanda Kosovo aliyefariki Jumamosi asubuhi, umeendelea kuteka hisia za watu wengi.

Ndanda anazikiwa Jumatano hii saa 9 mchana kwenye makaburi ya Kinondoni (Mwembejini) walikozikwa mastaa wengine kama Steven Kanumba, Adam Kuambiana, Martin Kasyanju na wengine wengi.

Watu wamekuwa wakiwasili kila wakati kwenye eneo la msiba Kinondoni Hananasif kwenye nyumba ya balozi wa Congo (DRC).

Ratiba kamili ya kamili ya mazishi ya Ndanda ni kama hivi:
Jumatano (13-APR-2016) saa 1 Asubuhi: Kwenda kuchukua mwili Muhimbili Hospital
Saa 4 asubuhi: Mwili kuwasili Kinondoni msibani.
Saa 6 Mchana: Chakula
Saa 7 mchana: Kuaga Mwili
Saa 9 mchana: Makaburini (Kinondoni)

Wageni wa heshima wanaotarajiwa kuhudhuria mazishi ni: Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda, Waziri wa Habari, Sanaa na Michezo Mh. Nape Nnauye, balozi wa Congo nchini Jean Pierre Mutamba na maafisa wote wote wa ubalozi wa Congo DRC.


PATA PICHA 18 ZA WATU WALIOKUWEPO MSIBANI JUMANNE USIKU
 Asha Baraka na Juma Mbizo
 Meneja wa Twanga Pepeta Hassan Rehani (kushoto) akiwa na Khamis Dacota wa Clouds FM
 Kutoka kushoto ni Pablo Masai, Doyi Moke na Joniko Flower
 Marapa G7  wa FM Academia na kulia ni Mirinda Nyeusi wa Mashujaa Band
 Kutoka kushoto ni Mirinda Nyeusi, Hassan Rehani na Haji BSS
 Jose Mara na Asha Baraka
 Baadhi ya waombolezaji wa kike waliofika msibani Jumanne usiku
 Wanenguaji wa FM Academia
  Mwimbaji wa FM Academia Malu Stonch ambaye aliingia Tanzania pamoja na marehemu Ndanda
 Kutoka kushoto ni Totoo ze Bingwa, Jose Mara, Juma Mbizo na Richard Mangustino
 Mahema yalivyokuwa yakitayarishwa
 Mule Mule FBI
 Kushoto ni Pishuu Meshaa akiwa na Steve
 Kushoto ni rapa Sauti ya Radi
 Comedian Steve Nyerere
 Mtangazaji wa Chanel Ten Sunday Mwakanosya
 Wadau
Baadhi ya waombolezaji



Comments