KIUNGO wa Arsenal, Mikel Arteta anaweza            kujiunga na Manchester City kama sehemu ya benchi la ufundi la            Pep Guardiola.
        Arteta mwenye umri wa miaka 34, atakuwa            nje ya mkataba mwisho wa msimu na amekusudia kustaafu na            kuhamia katika ukocha kiangazi hiki kutokana na matatizo ya            kuumia hivi karibuni.
        Licha ya kuwa nahodha, ushiriki wa kiungo            huyo Mhispania katika kikosi cha Arsene Wenger umezingirwa na            vikwazo katika kipindi cha misimu miwili ya mwisho kutokana na            idadi ya kuwa majeruhi, akicheza mechi nane za Premier League            msimu huu kwa sababu ya  kuendelea            kwa tatizo hilo.
        Arteta tayari amejipanga kuhamia katika            kufundisha soka na amekamilisha baadhi ya kozi za ukocha            katika chuo cha soka cha Arsenal.
        Guardiola anajiandaa kwenda na timu yake            ya ufundi Etihad Stadium kiangazi hiki wakati atakapochukua            nafasi ya Manuel Pellegrini, na chanzo cha habari kimeupasha            mtandao wa ESPN FC kwamba yu tayari kumpa ofa Arteta kuwa            miongoni mwa wasaidizi wake.
        Wawili hao waliopikwa pamoja katika kituo            maarufu cha soka cha Barcelona - La Masia wakiwa wachezaji            makinda, ni marafiki wa karibu.
        
Comments
Post a Comment