KOCHA ajaye wa Manchester City, Pep Guardiola ameripotiwa kutoa maelekezo kwa viongozi wa klabu hiyo kumsajili straika wa Borussia Dortmund, Pierre-Emerick Aubameyang kiangazi hiki.
Gazeti la Ufaransa la Le10 Sport limedai kuwa Manchester City itatumia zaidi ya pauni milioni 80 kuweza kumnasa sgtraika huyo mwenye miaka 27, ambaye pia anatolewa macho na Manchester United na Arsenal msimu huu akiwa na mabao yake 33.
Comments
Post a Comment