Pamoja na Kiwango Kibovu Uwanjani – Man Utd yazifunika Barca, Madrid, katika listi ya vilabu vyenye faida kubwa
Mauzo makubwa ya haki ya matangazo ya TV, mauzo ya jezi, mauzo          ya wachezaji na uuzaji, matangazo ya biashara na uuzaji wa          bidhaa mbalimbali zenye nembo za vilabu ni moja ya mambo          yaliyozitengenezea faida kubwa vilabu vya soka kwa muda wa miezi          zaidi ya 12 iliyopita.  
           Jarida la Forbes linalodili na masuala ya          biashara na fedha limechapisha listi ya vilabu 10 vilivyoingiza          faida kubwa duniani kote.
   Pamoja na matokeo yasiyoridhisha uwanjani,          klabu ya Manchester United imetajwa na jarida la Forbes la          Marekani kuwa klabu iliyoingiza faida kubwa zaidi kwa miezi 12          iliyopita. 
Listi kamili ya vilabu 10 vya soka vyenye faida kubwa.
1. Manchester United: $190 million
2. Real Madrid: $162 million
          3. Manchester City: $131 million
          4. Arsenal: $122 million
          5. Liverpool: $115 million
          6. Barcelona: $108 million
          7. Juventus: $81 million
          8. Tottenham Hotspur: $73 million
9. Schalke: $67 million
          10. Bayern Munich: $60 million
Comments
Post a Comment