Mechi ya Inter vs Udinese yavunja mwiko wa Serie A kwa kutohusisha mchezaji hata 1 wa kitailiano


Mechi ya Inter vs Udinese yavunja mwiko wa Serie A kwa kutohusisha mchezaji hata 1 wa kitailiano

Inter Milan wamefufua matumaini ya kupata nafasi ya kwenda kucheza soka la ulaya msimu ujao baada ya ushindi wa 3-1 dhidi ya Udinese juzi jumamosi.

  Katika mchezo huo Inter walifunga magoli yao kupitia Jovetic aliyefunga mawili na Mauri Icard akifunga lingine na kuifanya Inter kufikisha  pointi 64 wakishika nafasi ya 4 nyuma ya Roma wenye pointi 68, huku zikiwa zimebaki mechi 3 ligi kumalizika. 

  Mchezo huu wa Inter vs Udinese pia umeweka historia mpya katika Serie A, ligi ambayo ina sifa ya kukumbatia wachezaji wa kiitaliano. Mechi amya leo haijahusisha mchezaji hata mmoja raia wa Italia katika vikosi vyote viwili vilivyoanza kwa timu zote mbili. 

Hii haijawahi kutokea katika ligi ya Serie A tangu kuanzishwa kwake. 
Takwimu:  Inter Milan – Udinese 

 

Msimamo wa Ligi  

   



Comments