MARCUS RASHFORD AISHUSHA DARAJA ASTON VILLA ...atupia bao pekee, watamwelewa tu, Rooney arejea rasmi
Marcus Rashford kwa            mara nyingine tena anaibeba Manchester United baada ya            kuifungia bao pekee kwenye mchezo wa Ligi Kuu dhidi ya Aston            Villa kwenye uwanja wa Old Trafford.
        Kwa bao hilo la            dakika ya 32, Aston Villa wanashuka rasmi daraja ikiwa ni mara            yao ya kwanza ndani ya miaka 28 iliyopita.
        Aston Villa ina            pointi 16 ambazo hata kama ikishinda michezo yake iliyosalia,            haitawasaidia lolote.
        Marcus Rashford            mwenye umri wa miaka 18, alifunga bao hilo akiunganisha krosi            ya Antonio Valencia.
        Nahodha Wayne            Rooney alianza katika mchezo huo, akifanya hivyo kwa mara ya            kwanza tangu alipoumia katikati ya mwezi Februari.
        MANCHESTER              UNITED (4-2-3-1): De            Gea 6; Valencia 7.5, Smalling 6.5, Blind 6, Rojo 6;            Schneiderlin 6, Fellaini 6.5; Mata 6 (Fosu-Mensah 89), Rooney            6.5 (Lingard 67 6), Depay 7; Rashford 7 (Martial 76 6)
        ASTON              VILLA (4-4-1-1): Guzan 6; Hutton            5.5, Clark 6, Lescott 5.5, Cissokho 5.5; Sinclair 5.5, Bacuna            6, Westwood 6, Richardson 6 (Gestede 82 6.5); Gueye 6; Ayew            6.5
        Marcus Rashord              anashangilia bao lake
        Kitu kinatinga wavuni
        Dogo anapongezwa na              nahodha wake
        Wachezaji wa Aston              Villa hoi baada ya kushuka daraja
          
Comments
Post a Comment