MANCHESTER UNITED YATENGA MSHAHARA MNONO KWA NEYMAR ILI KUMNG'OA BARCELONA KWA ADA YA REKODI MPYA YA DUNIA
MANCHESTER UNITED imeripotiwa "kukaa mkao            wa kula" wakati Barcelona ikielezwa kuwa tayari kumwachia            straika wake nyota, Neymar aondoke katika klabu hiyo.
        Klabu hiyo ya England kwa muda mrefu            imekuwa ikimtamani Mbrazil huyo, na kwa mujibu wa ripoti            imekuwa ikiwasiliana na wawakilishi wake kuweka wazi kuwa iko            tayari kutimiza matakwa ya mkataba wake Barca kwa kulipa pauni            milioni 144.
        United pia iko tayari kumpa Neymar mwenye            miaka 24 ofa ya mshahara mnono wa pauni 300,000 kwa wiki kama            atakubali kuondoka Nou Camp na kutua Old Trafford.
        Straika huyo wa zamani wa Santos ya Brazil            kwa sasa anavuta mshahara wa pauni 77,000 kwa wiki Barca,            hivyo atapandishiwa karibu mara tatu zaidi kama ataamua            kuhamia United.
        Hata hivyo, The Sun limeripoti kuwa uamuzi            wa Neymar utategemea majaliwa ya United kama itafuzu Champions            League msimu ujao, kitu ambacho bado hakina uhakika kwa sasa            ambapo imeachwa nyuma pointi mbili na wapinzani wao wa mji            mmoja Manchester City katika mbio za kuwania 'top four'.
        Bado kuna matumaini kwa United kufanikiwa            dili hili wakati Barcelona ikihofia kutoweza kukidhi mahitaji            ya Neymar kifedha bila kuiweka klabu katika hatari, wakati pia            ikikabiliwa na kibarua cha kuwabakisha mastaa wengine kama            Lionel Messi na Luis Suarez kwa kuwapa mikataba mipya.
        
Comments
Post a Comment