MANCHESTER UNITED YAICHAPA EVERTON 2-1 NA KUTINGA FAINALI YA FA CUP ...Martial aibuka shujaa, Lukaku akosa penalti
Manchester United            imetinga fainali ya FA kwa mara ya kwanza tangu mwaka 2007            baada ya kuifunga Everton 2-1 kwenye nusu fainali iliyopigwa            katika dimba la Wembley.
        Marouane Fellaini            aliifungia United bao la kwanza dhidi ya timu yake hiyo ya            zamani kunako dakika ya 34.
        Kipindi cha pili            Everton ilipoteza nafasi nzuri ya kusawazisha pale Romelu            Lukaku alipopiga penalti iliyopanguliwa na kipa David De Gea.
        Hata hivyo dakika            ya 76 Chris Smalling alijifunga na kufanya matokeo yawe 1-1            hadi dakika za majeruhi ambapo Anthony Martial alikimbia na kuuwahi mpira            wa Ander Herrera na kufunga bao            la ushindi kwa United.
        United sasa            itaumana na mshindi wa Jumapili kati ya Crystal Palace na            Watford.
        Everton: Robles, Besic, Stones, Jagielka, Baines,            McCarthy, Gibson (Mirallas 90mins), Lennon (Deulofeu 70),            Barkley, Cleverley, Lukaku
        Manchester              United: De Gea, Fosu-Mensah (Valencia 62), Smalling,            Blind, Rojo, Carrick, Lingard, Fellaini (Herrera 87), Rooney,            Martial, Rashford
        Anthony Martial              akishangilia bao la ushindi alilifunga dakika za majeruhi
        Martial akiifungia              United bao la ushindi
        Nahodha Wayne Rooney              akishangilia baada ya mpira kwisha
        Louis van Gaal na              Anthony Martial wakifurahi baada ya mpira kumalizika
        Nyota wa Everton Gerard              Deulofeu na Tom Cleverley wakishangilia baada ya  Smalling              kujifunga na kuwa bao la kusawazisha
        Marouane Fellaini              akisherehekea bao lake dhidi ya timu yake ya zamani
          
Comments
Post a Comment