MANCHESTER UNITED YAICHAPA EVERTON 2-1 NA KUTINGA FAINALI YA FA CUP ...Martial aibuka shujaa, Lukaku akosa penalti



MANCHESTER UNITED YAICHAPA EVERTON 2-1 NA KUTINGA FAINALI YA FA CUP ...Martial aibuka shujaa, Lukaku akosa penalti
Marouane Fellaini glides away from Aaron Lennon during a            first half controlled by Manchester United for the most part
Manchester United imetinga fainali ya FA kwa mara ya kwanza tangu mwaka 2007 baada ya kuifunga Everton 2-1 kwenye nusu fainali iliyopigwa katika dimba la Wembley.

Marouane Fellaini aliifungia United bao la kwanza dhidi ya timu yake hiyo ya zamani kunako dakika ya 34.

Kipindi cha pili Everton ilipoteza nafasi nzuri ya kusawazisha pale Romelu Lukaku alipopiga penalti iliyopanguliwa na kipa David De Gea.

Hata hivyo dakika ya 76 Chris Smalling alijifunga na kufanya matokeo yawe 1-1 hadi dakika za majeruhi ambapo Anthony Martial alikimbia na kuuwahi mpira wa Ander Herrera na kufunga bao la ushindi kwa United.

United sasa itaumana na mshindi wa Jumapili kati ya Crystal Palace na Watford.

Everton: Robles, Besic, Stones, Jagielka, Baines, McCarthy, Gibson (Mirallas 90mins), Lennon (Deulofeu 70), Barkley, Cleverley, Lukaku

Manchester United: De Gea, Fosu-Mensah (Valencia 62), Smalling, Blind, Rojo, Carrick, Lingard, Fellaini (Herrera 87), Rooney, Martial, Rashford
Anthony Martial celebrates                  after scoring an injury-time winner to send Manchester                  United into the FA Cup final over Everton
Anthony Martial akishangilia bao la ushindi alilifunga dakika za majeruhi
Martial sends his effort                  beyond Joel Robles and into the back of the net to break                  Evertonian hearts at Wembley on Saturday
Martial akiifungia United bao la ushindi
Wayne Rooney celebrates                  after the final whistle as he keeps alive his dream of                  finally adding an FA Cup winner's medal to his tally
Nahodha Wayne Rooney akishangilia baada ya mpira kwisha
Louis van Gaal and Anthony                  Martial are joined together on the pitch after full-time                  as Manchester United basked in victory at Wembley
Louis van Gaal na Anthony Martial wakifurahi baada ya mpira kumalizika
Gerard Deulofeu and Tom                  Cleverley celebrate after Smalling's own goal brought                  them level in the FA Cup semi-final with 15 minutes                  left
Nyota wa Everton Gerard Deulofeu na Tom Cleverley wakishangilia baada ya  Smalling kujifunga na kuwa bao la kusawazisha
Marouane Fellaini celebrates                  after giving Manchester United the lead against Everton                  in Saturday's FA Cup semi-final at Wembley
Marouane Fellaini akisherehekea bao lake dhidi ya timu yake ya zamani



Comments