MANCHESTER CITY YATINGA NUSU FAINALI, YAIBANJUA PSG LIGI YA MABINGWA



MANCHESTER CITY YATINGA NUSU FAINALI, YAIBANJUA PSG LIGI YA MABINGWA

Manchester City imetinga nusu fainali ya Ligi ya Mabingwa baada ya kuibanjua Paris Saint Germain 1-0 kwenye dimba la Etihad.

City inapenya kwa jumla ya bao 3-2 kufuatia sare ya 2-2 ndani ya jiji la Paris wiki iliyopita. 

Shukran za dhati kwa mashabiki wa City zinakwenda kwa Kevin de Bruyne aliyefunga bao pekee dakika ya 76, hiyo ikiwa ni baada ya Sergio Aguero kukosa penalti dakika ya 30.


Comments