Manchester City imeanza kwa sare ya 0-0 kwenye uwanja            wake wa Etihad dhidi ya Real Madrid katika mchezo wa kwanza wa            nusu fainali ya Champions League.
        Hiyo inamaanisha kuwa katika mchezo wa marudiano wiki            ijayo, miamba hiyo ya England itahitaji sare yoyote ya magoli            ili kutinga fainali kwa faida ya goli la ugenini.
        Real Madrid wana mlima mrefu wa kupanda nyumbani kwani            ni lazima washinde mchezo huo, vinginevyo sare ya 0-0            italazimisha mshindi kupatikana kwa hatua ya matuta.
        Hata hivyo Real Madrid wanaweza wakawa na faida ya            uwepo wa Cristiano Ronaldo ambaye ameukosa mchezo wa kwanza            baada ya kocha wake Zinedine Zidane kuamua kuendelea kumlinda            kufuatia maumivu ya msuli aliyoyapata tangu wiki iliyopita.
        Awali Zidane alisema Ronaldo yuko fiti lakini mwisho wa            siku kocha huyo hakutaka kucheza kamari juu ya afya ya            mchezaji huyo tegemeo.
                                        
Comments
Post a Comment