MANCHESTER CITY HAINA MPANGO NA PAUL POBGA, YAHAMISHIA NGUVU KWA ALVARO MORATA



MANCHESTER CITY HAINA MPANGO NA PAUL POBGA, YAHAMISHIA NGUVU KWA ALVARO MORATA

MANCHESTER CITY ilitarajiwa kuweka mezani pauni milioni 80 kwa ajili ya kumrejesha England staa wa Juventus, Paul Pogba kiangazi hiki, lakini sasa haina tena mpango nae na badala yake inamtaka Alvaro Morata.

Gazeti la The Sun limedai kuwa City kwa sasa inaelekeza nguvu zake katika kumtwaa Morata – pia wa Juventus ili kuiongezea makali safu yake ya ushambuliaji.

Straika huyo wa kimataifa wa Hispania, amefunga mabao sita tu na kupika sita katika mechi 31 za Serie A msimu huu, huku zaidi ya nusu akifunga akitokea benchi kutokana na kukabiliwa upinzani wa namba kutoka kwa Simone Zaza na Paolo Dybala.

Licha ya kuwa Arsenal imekuwa ikimtamani kwa muda mrefu Morata mwenye miaka 23 na kutaka kumsajili kiangazi hiki, mtandao wa CalcioMercato umeripoti kwamba kocha ajaye Chelsea, Antonio Conte pia ni shabiki mkubwa wa straika huyo.

Kutokana na timu tatu za Premier League kuonyesha nia ya kumtaka straika huyo, Real Madrid inaonekana kujipanga kumnunua na kisha kumuuza kwa faida.


Morata aliondoka Madrid mwaka 2014, lakini klabu hiyo ya Hispania ina ubavu wa kumrejesha kwa pauni milioni 23.7 kulingana na mkataba walioingia na Juve.


Comments