LOUIS VAN GAAL ASEMA ZLATAN IBRAHIMOVIC AMEMKATISHA TAMAA


LOUIS VAN GAAL ASEMA ZLATAN IBRAHIMOVIC AMEMKATISHA TAMAA

LOUIS VAN GAAL amesema Manchester United haina mpango wa kumsajili straika wa Paris Saint-Germain, Zlatan Ibrahimovic, akidai kuwa umri wake wa miaka 34 ni mkubwa sana.

"Tunahitaji kuboresha uchaguzi wetu (wa kikosi), kwa sababu wakati nilipochukua timu tulikuwa na wachezaji sita au saba wenye umri juu ya miaka 33," Van Gaal alikiambia kituo cha TV Viasat ya Sweden.

Alisema alitazama mechi ya PSG na Manchester City ambapo alishangazwa na kilichofanywa na Ibrahimovic.

"Alinikatisha tamaa sana kwa sababu alipaswa kufunga angalau mara mbili," alisema.


Comments