LOUIS VAN GAAL AMLINGANISHA MARCUS RASHFORD NA PATRICK KLUIVERT



LOUIS VAN GAAL AMLINGANISHA MARCUS RASHFORD NA PATRICK KLUIVERT
Manchester United's            Marcus Rashford has netted seven goals in 13 appearances

LOUIS VAN GAAL amesema kuibuka kwa straika wake kinda Marcus Rashford, kunarandana na ilivyokuwa kwa Patrick Kluivert katika klabu ya Ajax Amsterdam ya Uholanzi.

Mholanzi huyo ambaye alikuwa kocha wa Ajax wakati Kluivert alipoibuka kwa mara ya kwanza na kutikisa katika Eredivisie, anadhani Rashford anaweza kufuata nyayo za straika huyo wa zamani wa Newcastle United.

Akiwa na mabao saba katika mechi 13 msimu huu, kinda huyo wa miaka 18 ametikisa katika Premier League wakati nyota wenzake wanaomzunguka wakihangaika kuwa kwenye kiwango.

"Ana umbile sawa na Patrick, lakini Patrick alikuwa vizuri sana katika uzito wa mwili, lakini nadhani hiyo ni sula la muda tu kwa Rashford," alisema van Gaal.
 "Lakini vipi alikuwa Kluivert katika mwaka wangu wa kwanza Ajax ndivyo ilivyo kwa Rashford sasa katika mwaka wangu wa pili United."

Kluivert alikwenda hadi kucheza katika timu kama Barcelona na AC Milan, sambamba na kufunga mabao 40 katika mechi 79 alizoichezea timu ya taifa ya Uholanzi.


Comments