Kocha Jurgen Klopp ameibana timu yake ya zamani - Borussia Dortmund baada ya Liverpool kulazimisha sare 1-1 katika mchezo wao wa kwanza wa robo fainali ya Europa League.
Mshambuliaji Divock Origi aliifungia Liverpool bao la kuongoza dakika ya 36, lakini nahodha wa Dortmund Mats Hummels akaisawazishia timu yake dakika ya 48.
Kwa kufunga bao la ugenini, Liverpool inajiweka sehemu nzuri zaidi katika mchezo wao wa marudiano utakaofanyika Anfield wiki ijayo.
Matokeo ya mechi zingine za Europa League ni:
Athletic Bilbao 1 - 2 Sevilla
Braga 1 - 2 Shakhtar Donetsk
Villarreal 2 - 1 Sparta Prague
Mshambuliaji wa Liverpool Divock Origi (katikati) akipongezwa na wenzake baada ya kuifungia Liverpool bao la kuongoza dakika ya 36
Jurgen Klopp akishangilia bao dhidi ya timu yake ya zamani
Nahodha wa Dortmund Mats Hummels (kulia) akishangilia baada ya kumtungua kipa Simon Mignolet kwa mpira wa kichwa
Comments
Post a Comment