LAURENT BLANC            ameingizwa ghafla kwenye mbio za kuikochi Manchester United            msimu ujao, nafasi ambayo kimahesabu ni kama tayari iko            mikononi mwa Jose Mourinho.
        Inasemekana kuna            dalili kubwa ya bodi ya Manchester United kusapoti kuchukuliwa            kwa Blanc anayeifundisha Paris            Saint-Germain.
        Blanc, sentahafu            wa zamani wa Ufaransa, aliimalizia soka lake Manchester United            kati ya mwaka 2001 na 2003.
        The Sun la            Uingereza linaandika kuwa sababu kubwa ya kutajwa kwa Blanc ni            kumlinda Ryan Giggs.
        Inaaminika kuwa            Mourinho atatua United benchi lake lote la ufundi na kumpiga            chini Giggs mwenye historia ya kipekee Old Trafford.
        Hata hivyo kwa            upande wa Blanc haitakuwa tatizo kwake kufanya kazi na Giggs            aliyecheza naye pamoja kwa misimu miwili Manchester United.
        Bado hakuna            habari rasmi kuwa dili la Mourinho kwenda United limeyeyuka            ambapo inaaminika kuwa makubaliano ya awali ya mkataba wa            pauni milioni 6o yameshafanyika kwa Mreno huyo kumrithi Louis            van Gaal.
                Paul Scholes,              Laurent Blanc na Ryan Giggs walipokuwa wakiitumikia              Manchester United mwanzoni mwa miaka ya 2000
        

Comments
Post a Comment