Kocha            wa kikosi cha Chelsea Guus Hiddink amesema kiungo wa timu hiyo            Eden Hazard yuko kizani msimu huu.
        "Msimu uliopita ulikua            mzuri sana kwake, na kila kitu kilienda sawa lakini msimu huu            kila kitu kwake kimekua kiza," alisema kocha huyo wa muda wa            timu.
        Katika msimu huu kiungo            huyu amefunga mabao mawili tu katika michuano ya kombe la Fa            huku akiwa hajazifumania nyavu katika michezo ya ligi kuu.
        Hazard,mwenye umri wa            miaka 25, alichaguliwa kuwa mchezaji bora wa mwaka wa (PFA)            Mwaka 2015.
        Kiungo huyu amebakiza            miaka minne katika mkataba wake na miamba hao wa Stamford            Bridge ila amekua akihusishwa na kuhama mwishoni mwa msimu            huu.
        
Comments
Post a Comment