JOSE MOURINHO bado ana matumaini kwamba            atakuwa kocha wa Manchester United mwisho wa msimu na            ameripotiwa kupanga kufanya usajili wa mastaa watano kiangazi            hiki.
        Kocha huyo Mreno amekuwa na matumaini ya            kutua Old Trafford baada ya msimu mbovu chini ya Louis van            Gaal ambaye pia anaamini kuwa ataendelea kulinda kibarua            chake.
        Kwa mujibu wa mtandao wa ESPN, Mourinho            anaamini mipango yote ya yeye kutua Old Trafford ipo kwenye            mstari na kilichobakia ni suala la muda tu.
        Majuzi akiongea na Sky Sports, Mourinho            alisema msimu ujao atakuwa na timu mpya na kwamba matarajio            yake kuendelea kufundisha Premier League.
        
Comments
Post a Comment