Kocha huyo wa            Kireno anapewa nafasi kubwa ya kumrithi Louis van Gaal ndani ya Manchester United            msimu ujao iwapo Ed Woodward            ataamua kusitisha kibarua cha Van Gaal.
        Na sasa utashi wa            Mourinho  katika usajili wake wa kwanza unaweza kuwa ni wa Lewandowski - hiyo ni kwa mujibu wa ujumbe            wa simu ya mkononi aliomtumia mchezaji huyo miaka mitatu            iliyopita.
        Manchester Evening News inadai Mourinho            alimtumia ujumbe huo mshambuliaji huyo wa Bayer Munich (enzi            hizo akiichezea Borussia            Dortmund) baada ya kufunga mara nne dhidi ya Real Madrid            kwenye Champions League mwaka 2013. Mourinho ndiye aliyekuwa            kocha wa Real Madrid kipindi hicho.
                
Comments
Post a Comment