HAWA NDIO MAKOCHA WANAOTAJWA KUMRITHI ARSENE WENGER NDANI YA ARSENAL



HAWA NDIO MAKOCHA WANAOTAJWA KUMRITHI ARSENE WENGER NDANI YA ARSENAL
Wenger's contract at the Emirates Stadium is due to            expire next summer and he has hinted at leaving then

Bosi wa Southampton Ronald Koeman yuko miongoni mwa majina ya makocha wanaotajwa kumrithi  Arsene Wenger ndani ya Emirates Stadium.

Wenger amebakiza mwaka mmoja kwenye mkataba wake Arsenal lakini sasa kumeibuka shinikizo kubwa linalotishia kung'oka kwa kocha huyo mwishoni mwa msimu huu.

Kwa mujibu wa The Sun la Uingereza, Arsenal imeanza kumulika watu wanaofaa kumrithi Wenger ambapo Koeman anaongoza orodha hiyo.
Koeman amefanya kazi nzuri Southampton tangu alipomrithi Mauricio Pochettino mwaka 2014.
Mdachi huyo naye anaingia mwaka wa mwisho katika mkataba wake Southampton lakini klabu hiyo inataka kumpa mkataba mpya wa muda mrefu.
Kocha wa Atletico Madrid - Diego Simeone na Laurent Blanc wa PSG nao ni miongoni wa mabosi wanaotajwa kutua Emirates Stadium.



Comments