GARETH BALE ASAFISHA HALI YA HEWA KATI YAKE NA RONALDO


GARETH BALE ASAFISHA HALI YA HEWA KATI YAKE NA RONALDO
Nyota wa Real Madrid Gareth Bale amezima hisia kuwa amewahi kukwaruzana na Cristiano Ronaldo kwa kusisitiza kuwa mchezaji mwenzake huyo amemsaidia sana katika kuzoea maisha ya Hispania.

Baadhi ya vyombo vya habari mara kadhaa vimekuwa vikimhoji Bale juu ya uhusiano wake na Ronaldo uwanjani na nje ya uwanja, lakini raia huyo wa Wales hakuwa lolote zaidi ya kusema kamwe hawakuwahi kuwa na mzozo.

Bale alitua Real Madrid mwaka 2013 akitokea Tottenham kwa ada ya rekodi ya dunia ya pauni milioni 86, lakini mara kadhaa ilidaiwa kuwa aliwahi kushutumiwa na Ronaldo kwa uchoyo wa pasi.

Katika mahojiano yake na The Times, Bale alisema: "Ronaldo anazungumza Kiingereza na alinisaidia sana nilipofika hapa. Tulikuwa pamoja kwenye Premier League na hivyo ilikuwa rahisi kwetu kuwa na mawasiliano mazuri.

"Vyombo vya habari vimekuwa vikisema vitu vingi ambayo wakati mwingine havikuwahi kutokea. Sikuwahi kulumbana nae. Ni mtu mwema uwanjani - kila mtu anajua hilo, wakati mwingine watu wanamtafsiri ndivyo sivyo. Hatuna tatizo hata kidogo."
Former Tottenham star Gareth                  Bale (centre) insists he does get on with team-mate                  Cristiano Ronaldo (right)
 Gareth Bale (katikati) akishangilia na Cristiano Ronaldo (kulia)
Bale (pictured just a couple                  of months after arriving) says Ronaldo helped him settle                  at Real Madrid
Bale na Ronaldo 
The Welsh ace (right)                  believes the media have exaggerated moments when it has                  looked like they do not get on
Bale (kulia) anasema hana bifu na Ronaldo (kulia)





Comments