Nyota wa Real            Madrid Gareth Bale amezima hisia kuwa amewahi kukwaruzana na            Cristiano Ronaldo kwa kusisitiza kuwa mchezaji mwenzake huyo            amemsaidia sana katika kuzoea maisha ya Hispania.
        Baadhi ya vyombo            vya habari mara kadhaa vimekuwa vikimhoji Bale juu ya uhusiano            wake na Ronaldo uwanjani na nje ya uwanja, lakini raia huyo wa            Wales hakuwa lolote zaidi ya kusema kamwe hawakuwahi kuwa na            mzozo.
        Bale alitua Real            Madrid mwaka 2013 akitokea Tottenham kwa ada ya rekodi ya            dunia ya pauni milioni 86, lakini mara kadhaa ilidaiwa kuwa            aliwahi kushutumiwa na Ronaldo kwa uchoyo wa pasi.
        Katika mahojiano            yake na The Times, Bale alisema: "Ronaldo anazungumza            Kiingereza na alinisaidia sana nilipofika hapa. Tulikuwa            pamoja kwenye Premier League na hivyo ilikuwa rahisi kwetu            kuwa na mawasiliano mazuri.
        "Vyombo vya habari            vimekuwa vikisema vitu vingi ambayo wakati mwingine havikuwahi            kutokea. Sikuwahi kulumbana nae. Ni mtu mwema uwanjani - kila            mtu anajua hilo, wakati mwingine watu wanamtafsiri ndivyo            sivyo. Hatuna tatizo hata kidogo."
         Gareth Bale (katikati)              akishangilia na Cristiano Ronaldo (kulia)
        Bale na Ronaldo 
        Bale (kulia) anasema              hana bifu na Ronaldo (kulia)
        
Comments
Post a Comment