SHABIKI wa Barcelona, Curvy Suzy Cortez,            ambaye ni mshindi wa shindano la urembo la Miss BumBum Brazil            2015, amedai kuzuiwa kuingia katika ukurasa wa Instagram wa            Lionel Messi kutokana na wivu wa mpenzi wa staa huyo,            Antonella Roccuzzo.
        Kwa mujibu wa gazeti la The Sun, mrembo            huyo mwenye miaka 25, amekuwa akitupia picha kibao zenye            ushawishi wa mapenzi kwenye ukurasa huo wa Instagram            zinazotafsiriwa kuwa na lengo la 'kumtega' Messi.
        Katika moja ya picha hizo, mwanamitindo            huyo Mbrazili anaonekana amepozi na jezi ya Barcelona, huku            akiwa amevaa chupi nyembamba iliyogawa makalio yake,            akimpongeza Messi kwa kushinda tuzo yake ya tano ya mwanasoka            bora wa dunia.
        Picha nyingine, inamwonyesha Suzy akiwa            amepozi 'nusu-uchi' huku akiwa amevaa kofia ya Barcelona na            kuweka juu ya bega lake viatu vya soka vya Messi vyenye nembo            ya Adidas.
        Kwa mara nyingine tena, Suzy alionekana            pichani akionyesha maumbile yake, akiwa amevaa jezi maarufu            namba 10, akivinjari kwenye pwani ya Ureno.
        Mrembo huyo licha ya kumshambulia            Antonella kwamba ana wivu na amechukua hatua kali kwa picha            zake zenye mvuto wa mahaba, alijitetea kuwa yeye ni shabiki            mkubwa wa Barcelona na hakuna cha zaidi.
        Suzy ambaye anajulikana nyumbani kwao            Brazil kwa sifa yake ya kupenda "kutoka" na wanasoka alisema:            "Nilishtushwa wakati nilipobaini hili. Kama ningaliweza,            ningalimwambia asiwe na wasiwasi juu yangu, mimi ni shabiki            tu. Nilishangaa kwamba yeye mwenyewe hana uhakika zaidi.
        "Nadhani inaweza kuwa ni kwa sababu tu ana            wivu. Ni mbaya sana kwa sababu mimi ni shabiki tu wa soka na            shabiki mkubwa wa Barcelona." 
        Messi na Antonella ni wapenzi wa tangu            utotoni na walijuana wakati wakiwa na umri wa miaka mitano.            Wawili hawa walikulia katika mji mmoja nchini Argentina na            wakabaki kuwa marafiki hata baada ya Messi kwenda kufanya            majaribio Barcelona.
        Wawili hawa walijitambulisha rasmi kuwa            wapenzi mwaka 2009 na sasa wana watoto wawili.
        
Comments
Post a Comment