CHELSEA imekuwa ikihusishwa na uhamisho wa            Paul Pogba na Leonardo Bonucci wa Juventus, na Mkurugenzi Mkuu            wa miamba hiyo ya Serie A, Beppe Marotta amebainisha kuwa dili            linaweza kufanyika kati ya klabu hizo mbili.
        Marotta ameripotiwa akisema kuwa anataka            kufanya biashara na Chelsea kiangazi hiki kufuatia kuwasili            kwa kocha Antonio Conte katika klabu hiyo ya Stamford Bridge.
        Conte alishinda mataji matano ya Serie A            akiwa mchezaji wa kiungo Juve kabla ya kuiongoza kushinda            mataji matatu mengine akiwa kocha, na Marotta amesisitiza kuwa            anafurahia kumuona Mtaliano huyo akipata kazi katika Premier            League.
         "Sisi na            Chelsea tunaheshimiana," aliiambia Radio Rai. "Tunaona fahari            kwamba Conte sasa ni kocha wao… Ni jambo ambalo tunaweza            kujivunia, kama sisi tulijitoa mhanga miaka mitano iliyopita            wakati tulipomkabidhi kuiongoza Juventus… Natumaini tutaweza            kufanya kazi pamoja katika soko la usajili."
        Hata hivyo, Marotta, haraka akathibitisha kwamba            uhusiano wa heshima hautakwenda mbali kiasi cha kutosha            kuwauzia Pogba.
        
Comments
Post a Comment