CESC FABREGAS ASEMA ATACHUKIA TOTTENHAM IKITWAA UBINGWA ENGLAND …aiombea dua Leicester



CESC FABREGAS ASEMA ATACHUKIA TOTTENHAM IKITWAA UBINGWA ENGLAND …aiombea dua Leicester

KIUNGO wa Chelsea raia wa Hispania, Cesc Fabregas, ameeleza wazi kuwa hataki kuona Tottenham ikishinda taji la Premier League msimu huu.

Tottenham imeachwa pointi tano nyuma ya Leicester baada ya kuibamiza 4-0 Stoke City Jumatatu usiku, na kubaki kuwa timu yenye uwezekano zaidi wa kuzima ndoto za vinara hao wa ligi.

Hata hivyo, akizungumza akiwa mchambuzi mwalikwa katika televisheni ya Sky Sport wakati wa mechi ya Spurs na Stoke, Fabregas alisema angependa Leicester kukamilisha historia yao kwa kushinda taji hilo.

Fabregas aliwahi kuichezea Arsenal, ambayo ni mpinzani mkubwa wa Spurs jijini London, kabla ya kuhamia Chelsea ambayo pia inatoka katika jiji hilo.


Comments