BARCELONA imeripotiwa kumfukuzia kipa wa            Bayer Leverkusen, Bernd Leno kwa ajili ya kuziba nafasi ya            Marc-Andre ter Stegen, ambaye anaelezwa kuwa njiani kuondoka            Bundesliga katika usajili wa kiangazi hiki na kuhamia La Liga            au Premier League.
        Hata hivyo, Barca inatakiwa kuchangamka            kama inataka kumpata Leno kwa bei nafuu.
        Kipa huyo Mjerumani aliye chaguo la pili,            kwa mujibu wa mkataba wake wa sasa unaofikia kikomo Aprili 30,            klabu inayomtaka italazimika kulipa euro milioni 16.25.
        Zimebaki siku chache kufika Aprili 30,            hivyo Barca inatakiwa kukimbia na muda, kwani Leverkusen            inaweza kupandisha thamani ya kipa huyo mara mbili zaidi.
        Kipa huyo wa miaka 24 ambaye kwa mujibu wa            The Sun yuko mguu ndani mguu nje baada ya kutoelewana na kocha            wake, Roger Schmidt, amemvutia pia kocha wa Tottenham Hotspur,            Mauricio Pochettino lakini kuna uwezekano mdogo wa kukubali            kwenda kuwa nyuma ya Hugo Lloris.
        Barcelona inaonekana kuwa chaguo bora            kutokana na kutarajiwa kumruhusu Ter Stegen kuondoka mwisho wa            msimu, na hivyo kupambana na Claudio Bravo kwa ajili ya kuanza            kikosini.
        
Comments
Post a Comment