BARCELONA SAFARI IMEWADIA, YAPIGIGWA 2-0 NA ATLETICO MADRID NA KUTOLEWA CHAMPIONS LEAGUE ...BAYERN NAYO YASONGA
Barcelona imeshindwa kulinda              ushindi wake wa 2-1 ilioupata nyumbani kwake dhidi ya              Atletico Madrid wiki iliyopita na sasa imeaga michuano ya              Ligi ya Mabingwa.
        Miamba hiyo ya Hispania ikakubali              kichapo cha 2-0 katika mchezo uliochezwa Jumatano usiku na              kufungasha virago kwa jumla ya bao 3-2.
        Mabao yote ya Atletico yamefungwa              na Antoine Griezmann dakika ya 36 na 88.
        Atletico sasa inaungana na              Manchester City, Real Madrid na Bayern Munich katika hatua              ya nusu fainali.
        Bayern Munich imevuka kwenda nusu              fainali baada ya kutoka sare ya 2-2 na Benfica na hivyo              kuvuka kwa jumla ya 3-2 kufuatia ushindi wa 1-0 katika              mchezo wa kwanza.
        ATLETICO              XI: Oblak, Juanfran, Godin, Lucas, Filipe Luis,            Augusto (Savic 93), Gabi, Saul, Koke, Griezmann (Correa 90),            Carrasco (Partey 74) 
        BARCELONA              XI: Ter Stegen, Alves (Sergi Roberto 64), Mascherano,            Pique, Alba, Busquets, Rakitic (Arda Turan 64), Iniesta,            Neymar, Suarez, Messi 
        
Comments
Post a Comment