RATIBA ya hatua ya            mtoano ya timu 16 bora ya michuano ya Kombe la Shirikisho            Afrika imetoka ambapo Mabingwa wa Tanzania, Yanga wamepangwa            kucheza na GD Esperanca ya Angola.
        Yanga imeangukia katika            michuano hiyo ambayo ni ya pili kwa ukubwa Afrika baada ya            kufungwa na Al Ahly ya Misri kwa mabao 2-1 Jumatano usiku na            kutupwa nje ya Ligi ya Mabingwa Afrika kwa jumla ya mabao 3-2.            Mechi ya kwanza walitoka 1-1 Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
        Katika hatua hiyo,            Yanga wataanzia nyumbani kati ya Mei 6 na 8 kabla ya kuifuata            GD Esperanca katika mchezo wa marudiano kati ya Mei 17 na 18.
        Mechi nyingine: Al Ahli            Tripoli vs Misr Makkassa; Mamelodi Sundowns vs Medeama SC; Al            Merreikh vs Kawkab Marrakesh; TP Mazembe vs Stade Gabesien;            Etoile du Sahel vs CF Mounana na MO Bejaia vs Esperance Tunis.
        
Comments
Post a Comment