AUGUSTO FERNANDEZ WA ATLETICO MADRID ALIVYOZIMA MIPANGO YA BAYERN MUNICH



AUGUSTO FERNANDEZ WA ATLETICO MADRID ALIVYOZIMA MIPANGO YA BAYERN MUNICH

KAMA ulitazama mechi ya awali ya nusu fainali ya Champions League kati ya Atletico Madrid na Bayern Munich iliyopigwa Estadio Vicente Calderon Jumatano usiku, hautapata kigugumizi kukiri kuwa Augusto Fernandez ndiye aliyerahisisha ushindi kwa wenyeji.

Kiungo huyo wa ulinzi raia wa Argentina aliyeanzishwa na Diego Simeone badala ya Yannick Ferreira Carrasco, alikuwa msaada mkubwa katika kuibana Bayern Munich hadi ikashindwa kuwa na ufanisi katika eneo la kiungo.

Augusto alipiga pasi zake kwa ukamilifu wa asilimia 84, akidhihirisha kwamba anaweza pia kusambaza mpira kwa wenzake kama kiungo wa ulinzi, na alikamata nafasi ya pili nyuma ya Koke kwa kukimbia kilomita nyingi dimbani – kilomita 12.4.

Staa huyo alifanya kazi muda wote dimbani, na kuiwezesha Atletico kumaliza dakika 90 nyumbani Calderon bila nyavu zake kutikiswa kuelekea mechi ya marudiano Allianz Arena.


Kama Simeone ataamua kumwamini tena Augusto, na akafanikiwa kuwa kwenye kiwango cha juu kwa mara nyingine, Bayern Munich watakuwa na wakati mgumu kuweza kugeuza matokeo mechi ya marudiano Jumanne ijayo.


Comments