ATLETICO MADRID YAENDELEA KULISONGESHA LA LIGA, YAIFUNGA MALAGA 1-0 ...kocha Diego Simeone 'apigwa benchi' jukwaani



ATLETICO MADRID YAENDELEA KULISONGESHA LA LIGA, YAIFUNGA MALAGA 1-0 ...kocha Diego Simeone 'apigwa benchi' jukwaani
The Atletico Madrid            played celebrate together at theĀ Vicente Calderon stadium            following the opening goal

KOCHA wa Atletico Madrid, Diego Simeone amejikuta akimalizia kipindi cha pili jukwaani katika mechi ya La Liga waliyoshinda 1-0 dhidi ya Malaga katika dimba la Vicente Calderon Jumamosi jioni baada ya mpira wa pili kurushwa uwanjani.

Matokeo yalikuwa 0-0 wakati mechi ikielekea mapumziko, ambapo Malaga walionekana kufanya shambulizi la kushtukiza, lakini refa Antonio Mateu Lahoz akasimamisha mchezo baada ya mpira wa pili kuingia dimbani.

Haikujulikana mara moja nani aliyerusha mpira huo dimbani, lakini refa alionekana akizungumza na Simeone wakati timu zikitoka nje kwa mapumziko, na wakati mechi ilipoanza kipindi cha pili kocha huyo alikaa jukwaani.

Sheria za La Liga zinaeleza kwamba kocha mkuu atawajibika kwa tabia zitakazojitokeza katika benchi lake, hivyo Simeone anaweza kuadhibiwa iwapo aliyerusha mpira uwanjani alikuwa mmoja wa wasaidizi wake.


Atletico ilishinda mechi hiyo kwa bao la dakika ya 62 lililofungwa na mtokea benchi Angel Correa kwa shuti kutoka umbali wa yadi 20.
Angel Correa celebrates                  after scoring the opening goal of the game against                  Malaga on Saturday afternoon
Angel Correa akisharehekea bao lake
Correa (L) celebrates with                  Atletico Madrid's Argentinian assistant coach German                  BurgosĀ 
Correa (kushoto) akishangilia na kocha msaidizi German Burgos 
Atletico Madrid manager Diego Simeone celebrates from                the stands having been sent off in the clash
Kocha wa Atletico Madrid Diego Simeone akishangilia huku akiwa jukwaani baada ya kutolewa kipindi cha pili


Comments