Pep Guardiola ana            kazi nzito ya kuutumia vema mchezo  wa marudiano wa nusu            fainali ya Ligi ya Mabingwa ili kuepukana na nuksi ya kukomea            nusu fainali tangu alipoanza kuikochi Bayern Munich.
        Kibarua hicho            kigumu kinakuja baada ya Bayern kupokea kisago cha bao 1-0            kutoka kwa Atletico Madrid katika wa mchezo wao kwanza            Jumatano usiku.
        Hii ni mara ya tatu            mfululizo kwa Guardiola kutinga hatua ya nusu fainali akiwa na            Bayern Munich ambapo mara mbili zilozopita, alikomea hatua            hiyo ya nusu fainali.
        Timu hizo            zinarudiana Ujerumani Jumanne ijayo katika mchezo unaotarajiwa            kuwa mgumu kupindukia.
        Bao pekee la            Atletico lilifungwa na Saul Niguez kunako dakika ya 11.
        Saul Niguez              akishangilia bao lake
        Saul akipongezwa na              wenzake
        Kocha wa Atletico               Diego Simeone akitoa maelekezo
        Fernando Torres              aliikosesha Atletico bao la wazi dakika ya 75
        
Comments
Post a Comment