ATLETICO MADRID YAANZA VEMA NUSU FAINALI KWA KUICHAPA BAYERN MUNICH 1-0



ATLETICO MADRID YAANZA VEMA NUSU FAINALI KWA KUICHAPA BAYERN MUNICH 1-0
Pep Guardiola ana kazi nzito ya kuutumia vema mchezo  wa marudiano wa nusu fainali ya Ligi ya Mabingwa ili kuepukana na nuksi ya kukomea nusu fainali tangu alipoanza kuikochi Bayern Munich.

Kibarua hicho kigumu kinakuja baada ya Bayern kupokea kisago cha bao 1-0 kutoka kwa Atletico Madrid katika wa mchezo wao kwanza Jumatano usiku.

Hii ni mara ya tatu mfululizo kwa Guardiola kutinga hatua ya nusu fainali akiwa na Bayern Munich ambapo mara mbili zilozopita, alikomea hatua hiyo ya nusu fainali.

Timu hizo zinarudiana Ujerumani Jumanne ijayo katika mchezo unaotarajiwa kuwa mgumu kupindukia.

Bao pekee la Atletico lilifungwa na Saul Niguez kunako dakika ya 11.

Saul Niguez celebrates after                  giving Atletico Madrid the advantage in their Champions                  League semi-final against Bayern Munich
Saul Niguez akishangilia bao lake
Saul was joined by his                  jubilant Atletico team-mates after his goal set up a 1-0                  first leg advantage for the Spanish side on Wednesday                  night
Saul akipongezwa na wenzake
Atletico manager Diego                  Simeone calls on his team and their supporters to raise                  the tempo during their first leg victory on Wednesday
Kocha wa Atletico  Diego Simeone akitoa maelekezo
Fernando Torres aliikosesha Atletico bao la wazi dakika ya 75


Comments