ARSENE Wenger amepuuza stori kuwa            amemfanya staa wa Leicester City, raia wa Algeria, Riyad            Mahrez, kuwa lengo lake kuu katika mabadiliko makubwa            anayotarajia kufanya katika kikosi chake kiangazi hiki,            ikiwamo 'kufagia' wachezaji walioshuka kiwango.
        Inadaiwa Wenger aliachia nafasi ya            kumsajili Mahrez mwenye thamani ya pauni milioni 25 sasa            Januari 2014 kabla ya kujiunga na Leicester kwa ada ya pauni            400,000 akitokea Le Havre inayoshiriki Ligue 2 ya Ufaransa.
        Bosi huyo wa Gunners amekiri kuwa moja ya            sababu za kumwacha wakati huo ilikuwa ni kukwepa kukosolewa            kwamba 'amechukua mchezaji asiye na jina badala ya kulipa            pauni milioni 40 kwa mchezaji mwenye jina kubwa'.
        Klabu kibao kubwa za Ulaya ikiwamo            Barcelona, zinamtaka staa huyo wa miaka 25, lakini Wenger            amewaeleza rafiki zake kwamba kumsajili kiungo huyo            mchezeshaji ndiyo kipaumbele chake.
        Alipoulizwa kwenye mkutano wa              waandishi wa habari kama anamtaka nyota huyo, Wenger              alijibu: "Habana na hata kama namtaka siwezi kusema lolote              kwa muda huu".
        
Comments
Post a Comment