VAN GAAL 'AMPIGIA SALUTI' MARUCUS RASHFORD ...asema ana kila kitu cha mshambuliaji nyota


VAN GAAL 'AMPIGIA SALUTI' MARUCUS RASHFORD ...asema ana kila kitu cha mshambuliaji nyota
Louis van Gaal amekiri kuwa kinda wa Machester United Marcus Rashford  ana kila kitu anachostahili kuwa nacho mshambuliaji mahiri.

Kocha huyo wa United ameyasema hayo baada ya kinda huyo kuifungia timu yake bao pekee kwenye ushindi wa 1-0 dhidi ya mahasimu wao Manchester City.


Bao la dakika ya 16 la Rashford lilitosha kupunguza pengo la pointi kwenye Premier League kati ya United na City ambapo sasa Manchester United imeachwa kwa pointi moja tu. 

Van Gaal akakiri kuwa chipukizi huyo mwenye umri wa miaka 18 alijihakikishia namba mara tu alipomchezesha mchezo wake wa kwanza mwezi uliopita. Hadi sasa Rashford kishatupia mabao matano katika michezo nane aliyocheza.
Marcus Rashford claps hands                  with Louis van Gaal following Manchester United's 1-0                  win at Manchester City
Marcus Rashford akipongezwa na Louis van Gaal 
Rashford's 16th minute                  effort which he steered past Joe Hart was enough to give                  Red Devils victory
Rashford akiitungua Man City dakika ya 16
Rashford celebrates with                  United team-mates as victory moves the Red Devils to                  within a point of their rivals
Rashford akipongezwa na wachezaji wenzake




Comments